Salaamu Watwana!
Mtunzi: ELlias K. Mwalongo
(Kanton)
SIMU: +255769313224,
E-Mail:mwalongoelias7@gmail.com
_______________________
Shukrani nyingi kwa Mungu
aliyeniumba na kuendelea kunipigania hadi siku hii ya leo. Tumaini langu ni
kwake pekee.
Wapendwa, wana wa ulimwengu huu
shupavu,ukipanda mahindi unatarajia kuvuna mahindi lakini pia unaweza usivune
ila huwezi kuvuna korosho! Majaribu katika maisha ni mtaji wa kujivunia maana
yamejaa utukufu na neema tele tele!
Ni vigumu sana kumzuia kuku
asitage, hata ukimfungia mlango atataga tu hata kama ni porini. Hivyo hakuna
anayeweza kuzuia mipango ya Mungu ndani ya maisha yako.
Wapendwa, msione kuku kachinjwa
mkaanza kumparamia mjinome minofu, hali hamjui ni visu vingapi vimemchinja kuku
huyo. Vingine huwa vina kutu, mtapata tetenasi bure.
Si kila mnachokiona kinang`aa
mkadhani kipya, vingine ni vibovu kabisa ila vimepakwa rangi tu ili kuficha
ubovu wake na kukuvutia wewe. Angalieni wapendwa msije mkaruka mwiba mkakanyaga
msumari, halafu make chini hatakama kuna tope.
Ya dunia ni mengi, mengine
hayawahusu. Kazaneni na yanayowahusu, maana kushuparia yasiyowahusu mtachelewa
kufanya yanayowahusu.
Muweni makini na wale wanaokalia
vigoda na kuanza kuhadithia ya wenzao, maana utakapoondoka watawawahathia
wengine ya kwako. Tena hawajazoea kusema ya kweli. Ukweli wanaupotezea, uongo
na uzushi mara moja utafika mtaa wa saba. Mbaya zaidi, yao wanayatia mfuniko na
ya wenzao wanayachezea mdundiko.
Wacha nifunge ginywa langu niache
kubwabwaja, lakini kabla sijakoma, wacha nimalizie aya hii moja ya mwisho.
Wapendwa, tufanye kazi. Kazi ni
kazi. Usidharau kazi ya mwenzako hali humchangii hata mia ya kula, wala hujui
anavaa nini au anakula nini na maisha yake yanaenda vipi. Tuheshimu kazi zetu
na kazi za wenzetu. Tuongeze juhudi katika kazi, kupata na kukosa ni matokeo ya
juhudi zetu, tusikate tamaa.
NAWATAKIENI KILA LILILO JEMA NA
KUDRA ZA MWENYEZI ZIWE MHIMILI WA MAISHA YETU SOTE.
_________AHSANTENI_________
Maoni na ushauri wako ni mhimu sana kwangu kusonga mbele.

No comments:
Post a Comment