KAZI YANGU
I T A N I L I S H A
(DIWANI
YA KANTON)
ISBN 978 9976 67 189 6
~~~~~~+++~~~~~~
MTUNZI;
Elias K. Mwalongo
(Kanton)
KAZI YANGU ITANILISHA
@Copyright by: Elias K. Mwalongo
S. L. P 977 Njombe
0769313224
Facebook: Elias Mwalongo
Twitter: Elias Mwalongo
Instagram: @mwalongoelias
Wahariri
1.Pd. Lucas Komba
Seminari Kuu Peramiho
2. Frt.Witney Selig Ngahi
Seminari Kuu Peramiho
3. Ndg. Oswald Ngonyani
Mhariri Mkuu Peramiho Publications
Kimechapwa Na;
Kanton Printing
S.L. P 977 Njombe
0769313224
Chapa Ya Kwanza, Februari 2016
Haki zote
zimehifadhiwa.Huruhusiwi kuiga, kupiga chapa, kutafsiri au kukitoa kitabu hiki
kwa jinsi yoyote ile pasipo idhini ya mwandishi wa kitabu hiki au mhariri
mhariri wake.Hatua za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayehusika.
***
Diwani yangu hii
ya KAZI YANGU ITANILISHA, nimeiandika
kwa heshima ya wale wote ambao wamekuwa wakinihamasisha katika fani hii ya
uandishi. Naamini wao ndio walionitia moyo hata nikafikia hapa. Ningetamani
kuwaandika majina yao yote katika ukurasa huu maana ninawakumbuka vema, lakini
hilo sitaliweza, hivyo nitajitahidi niandike baadhi yao tu ambao ni:
Pd. Atanas Mgimba
Pd. Ladislaus Mgaya
Frt. Sergio Kaberege
JohnBaptist Ngatunga
Dotto Rangimoto Chamchua
Gasto Mtitu
Godfrey Songolo
Joseph Chatanda
Simon Mgaya
Eligia Mwalongo
Antonia Mtega
***
+Katika makao ya milele mbinguni,
Astarehe kwa amani baba yangu mpendwa;
KALISTUS MWALONGO,
aliyenitoka
mwaka 2002 ningali siwezi kujikimu.
***
KAZI YANGU
ITANILISHA ni kitabu kinachopembua kwa uzito masuala
nyeti ya maisha ya kizazi hiki. Katika kitabu hiki cha mashairi, kuna majibu ya
maswali mengi yanayomsakama Mtanzania wa leo. Masuala hayo ni kama vile kifo,
mapenzi, utandawazi, tamaduni na kadhalika. Wanazuoni mnaweza kupata pia mawazo
mengi juu ya umhimu wa kuwaheshimu wazazi,katika shairi la “Asante Sana
Mama”,”Asante Sana Baba” na “Asanteni Sana Wazazi”. Pia kuna umhimu wa kutokata
tamaa katika maisha,hasa unaposhindwa kupata mafanikio unayoyasumbukia kwa
mudda mrefu katika shairi la “Huenda Kesho N`tapata”
Nimeguswa pia na mashairi yanayoelezea juu ya
siasa zisizo na ukweli katika utendekaji wake na udanganyifu uliojaa na kutuama
katika siasa za nchi zetu zinazoendelea. Haya unayapata katika shairi la
“Msing`ate Kucha” na lile la “Nani Atatupa Pole”.
Hali kadhalika mtunzi wa kitabu hiki amefaulu kwa
kiasi kikubwa kabisa kujitawanya katika nyanja za msingi zinazomgusa
binadamu.Mambo ya kiroho,kijamii, na hata kisiasa yapo katika kitabu hiki.Mambo
ya utandawazi yanayowaharibu vijana na hata watu wazima na wazee wa nyakati
hizi yanaelezwa na kupewa ufumbuzi katika kitabu hiki. Kuacha tamaduni zetu
zilizofunzwa na wazee wetu na kukimbilia kuiga tamaduni za kigeni pasipo
kuelewa na kujielewa, ni janga kwa jamii zetu.
Basi mpendwa msomaji, uhondo ndio huu. Yapo mengi
sana yatakayokufaa wewe katika maendeleo chanya ya fikra na hata katika nyanja
za kisiasa kiroho na hata kijamii. Kwenu ninyi nyote, yaliyomo humu ni mchango
mkubwa katika mabadiliko muhimu kwako na kwa nchi yetu.Yapo mengi ya kuwafaeni
katika maisha toka kitabu hiki cha KAZI YANGU ITANILISHA.
Na;
Frt. Witney Selig Ngahi
Seminari Kuu Peramiho
UTANGULIZI
Ni ukweli usiopingika kuwa katika maisha yetu hapa
duniani tunatofautiana kwa kiasi kikubwa hasa katika kujikimu.Wapo watu wengine
ambao hali zao kiuchumi ni njema, mifuko imetuna, chakula nyumbani hakipigi
chenga tena chakula kizuri.Wapo wanaotinga suti za bei mbaya na kutundika tai shingoni,viatu vya kiwi vilivyochongoka
mbele.Wana masimu makubwa, ya kupangusa. Hawatembei kwa
miguu,wanamashangingi na maprado ya kufa
mtu. Wanakunywa vinywaji vya gharama sio ulanzi wa shilingi mia nne kama
tunavokunywa sisi. Sawa ni vyao na wala tusiwaonee kijicho.Lakini wapo wenzangu
na mimi kapuku kabisa, tukibahatika kula leo hatuna uhakika wa kula kesho.
Mavazi yetu ndo usiseme, ni aibu tupu mbele za watu. Hatujali kwa kulala
ilimradi ikifika kesho na sisi tuwe bado tunapumua. Sisi ambao huenda
tunastahili hata kuitwa majina mabaya kama vile machokoraa. Sisi ambao mtu
akitupatia lifti japo kwenye baiskeli wakati wa jua kali la kiangazi tunamwona
ni mkombozi wetu, mtu akitupatia mihogo miwili tutafune wakati tuna njaa yetu
tunamwona ndiyo Mungumtu. Ni dhahiri thamani yetu ni duni sana mbele za
wenzetu.
Lakini
ndugu, licha ya tofauti hizi zote haimaanishi tubaguane, tugombane,
tusengenyane, tunyosheane vidole, tuzodoane au tudharauliane. Wapo watu
waliobobea na ambao ni hodari wa kujadili ya wenzao tena yasiyowahusu badala ya
kuendelea na yao. Yetu wanayachezea mdundiko yao wanayatia mfuniko. Kule kwetu
watu wa tabia hiyo wanaitwa Wambea. Waswahili wanasema, “Sitalia gizani kwa
kuwaogopa majirani”. Wambea shauri yao wenyewe, watakwisha kuni zao kwa
kunipikia machegea, wengine wamemaliza ndala zao kwa kutusimanga wongo mitaani.
Katika kuiandika Diwani yangu hii,nimegusa nyanja
mbalimbali za maisha. Lakini hasa nimejikita katika kuongelea kipato cha mtu
ambacho humfanya awe na maana mbele za watu au laa. Nimejaribu kuhamasisha kila
mmoja kukazana kujituma katika kazi yake ambayo ndiyo humpa shibe. Maana, MTU
KITU. Asiyekuwa na kitu hata thamani yake hutoweka, huonekana hana thamani
mbele ya wenyenavyo. Yapo yapo mambo yanayoweza kutufanya walau mara moja
tutabasamu lakini yanayotuliza ndio yamezidi. Lakini hatuna namna inatupasa
kupambana na pilika pilika za maisha haya hadi kieleweke, kwani wangapi
wamefanikiwa.
Zipo sera
zinaibuka kila kukicha hasa hapa kwetu Tanzania, na sisi ndio tunazishobokea na
kuzipigia makofi tukidhani zote zitatufaa. Wakisema “KILIMO KWANZA”
tunatabasamu na kupigia makofi. Lakini mbona somo la kilimo limefutwa darasani?
Tunasema tukuze vipaji vya vijana lakini somo la Stadi za Kazi shuleni tunalibeza
na kulifuta kwenye mitaala shuleni. Watu wa dini tofauti wanavyovurugana
wanapigana bunduki wanarushiana mikuki na kumwagiana tindikali tunashikilia
vichwa tunahuzunika, tunaita na vikao vya dharura hali Dini haifundishwi
mashuleni, watu hawashiki imani yao badala yake wanaleta ubabe.
Wanafunzi ndio
wasomi tunategemea mabadiliko katika jamii lakini wengi wao hamna kitu, miaka
inaisha anarudi kama alivyoenda, zaidi wanaongezeka miili na kuota ndevu. Je
wanafundishwa nini darasani? Kilimo? Hapana! Uchumi? No! Ujasiliamali? No,
kwanza haipo hata kwenye Silabasi.Watanzania
wenzangu, Mimi naona HAPA TUMECHEZA FYONGO!
Mimi
nisikuchoshe jisomee mwenyewe ufaidi uwasimulie na wenzako mambo yamo ndani ya
kitabu hiki. Ukimaliza kusoma kitabu hiki bila shaka utatamka pamoja nami kuwa
KAZI YANGU ITANILISHA.
Na;
Elias K. Mwalongo (Kanton)
Ruaha Catholic University
ILI KUPATA NAKALA HALISI YA KITABU HIKI WASILIANA NA MWANDISHI KWA SIMU NO. +255769313224
UTAMJULISHA ULIPO NAYE ATAKUELEKEZA NAMNA YA KUKIPATA.
ASANTE SANA