HATUANDIKI UPUMBAVU!!
Mtunzi na Mwandishi
ELIAS KALISTUS MWALONGO
(KANTON)
RUAHA CATHOLIC UNIVERSITY(RUCU)
+255769313224
@2017
Mpendwa
Muungwana na mzalendo wa nchi hii,
SALAAMU……………………!
Tukiwa
tunaelekea kuumaliza mwaka huu 2016, na tukiwa tumejaa matumaini ya kuanza
mwaka mwingine 2017 kwa amani, naomba nitumie fulsa hii adimu kutoa tathmini
yangu juu ya fani ya uandishi.
Ninajikita katika fani hii maana ndio kipaji alichonijalia mwenyezi, lakini
sasa fani hii hasa hapa kwetu Tanzania naona imebutuliwa mateke inachechemea
huenda tukaiua sisi wenyewe, kwakuwa hatusomi walivyoandika wenzetu na
kuvitendea kazi, na hasa kama mwandishi unamfahamu ndio kabisa anabezwa na kazi
yake hainunuliwi,haisomwi na hatimaye anakata tamaa.
Mpendwa,
unatuchukuliaje sisi tunaochukua kalamu, tukaketi chini na kuwaandikia tungo
zetu(MASHAIRI, SIMULIZI,TENZI, MAKALA n.k) kwa mfano mimi je,unanichukuliaje?
Ukisikia safari hii nimetunga kitabu kinaitwa MACHO YANGU YANANIDANGANYA, je wewe unanichukuliaje?
Nakuhakikishia
kwamba sisi waandishi hatupotezi muda tukakaa chini halafu tuandike UPUMBAVU.
Hata kama tunafahamiana na daima maongezi yetu kila siku ni ya kawaida kabisa
lakini mwenzio ninajambo ninaloliweka katika maandishi, naomba uniunge mkono.
Sidhani kama kuna mtu atajitetea hapa, wewe mwenyewe unayesoma makala hii ni
mvivu mkubwa wa kusoma kazi za wenzako. Ukiona Whatsup, au Facebook mtu
ameandika maelezo marefu unapotezea, je unadhani huyo mwenzako ameandika
UPUMBAVU. Ametumia muda akakuandikia habari hiyo ikufikie, wewe unasababu gani
ya kupotezea? Kila siku unalalamika maisha magumu, wanajitokeza watu wanaandika
mbinu za kujinafuu na ugumu wa maisha wewe unapotezea tu kama kawaida yako.
Ndugu yangu, hebu acha dharau hizo, sisi HATUANDIKI UPUMBAVU.
Unatamani
kujitetea? Kama nimekuonea nipigie simu namba hii +255769313224, au kama upo
Iringa hapa njoo tuonane ujitetee. Lakini kabla hujachukua uamuzi huo wacha
nikudhihirishie kuwa sisi waandishi umetudharau sisi na vyote tunavyoviandika,
hebu nambie kama umesoma vitabu vifuatavyo: Kama ndio njoo jitetee nitakununulia mirinda ya baridi,
na kama sio ukome kutudharau sisi waandishi…!
Je
umewahi kukiona na kukisoma kitabu kiitwacho JINSI JINI ALIVYOLISUMBUA PENZI LANGU kilichotungwa na GODWILL
SANGA wa chuo kikuu cha KAMPALA –Dar?
Je
umewahi kusoma vitabu viitwavyo “MARAFIKI NA MAADUI WA WATOTO” na “BORA KUWA
KOBE” vilivyotungwa na Frt. Isaya Nyambo wa SEMINARI KUU PERAMIHO?
Tena,
umewahi kusoma mashairi mazuuuuri yaliyopo katika kitabu kilichotungwa na EZRA
ESSAU MHONDA kiitwacho “JASHO NA MACHOZI YA DAMU YALINITOKA?
Umewahi
hata kukiona tu Kitabu kilichotungwa na binti mdogo tu YUSTINA DANDA, amehitimu
kidato cha nne mwaka huu, simulizi nzuri ya kusisimua iitwayo FURAHA BAADA YA
MACHOZI?
Bado,
Je umewahi kusoma simulizi yoyote kati ya hizi, “THE ADVENTURE OF ANALIZE,” au
“TUNDU LA KAA” zilizotungwa na katoto kadoooogo kabisa ka kidato cha tatu huko
St.Monika-Njombe. Au kama kawaida yako kudharau huhitaji hata kununua kakitabu
ka-shilingi 2000 tu ukafaidika kimaisha? Kwani viroba bei gani? Castle lager
nayo bei gani?, sigara je? Au unadhani
huyu mtoto ameandika UPUMBAVU.
Kama
hiyo haitoshi, hata vitabu vyangu mwenyewe je umewahi viona? Au ukisikia
matangazo ya vitabu vyangu unanibeza, hutamani hata kuviona unadhani nimeandika
UPUMBAVU?.
Umewahi
kusoma kitabu change kipi kati ya hivi, MACHO UANGU YANANIDANGANYA, DAMU YANGU
IMEMWAGWA NA MAMA`NGU, KARAHA TUPU!, MORE THAN A FRIEND, OLE WAKO MIMI
NIFUKUZWE SHULE NITAKUFA NA MTU, WHO CARE?, GAUNI LA MTUMBA, HAPA TUMECHEZA
FYONGO?
Hafu
wacha nisisahu, umewahi hata kusoma makala zangu magazetini? Yani hukomi tu
kutudharau sisi waandishi?
Wengine
wakiona nimevaa suti wanajua nimeuza vitabu vingi nimenunua suti! Ebo!
Wakiona
nakula mnofu wanajua nimeshauza kitabu cha KARAHA TUPU nimepata bukumbili ndo
najivinjari. Ebo!
Wengine
ni wivu tu, kitabu anatamani lakini akinunu anadhani mimi nitajenga mjengo kisa
buku jero yake ya kitabu cha OLE WAKO MIMI NIFUKUZWE SHULE, kwahiyo hanunui ili
kunikomoa. Kazi bure!
Wapendwa,
mwaka huu unaelekea ukingoni, sawa tu. Mwenyezi atujalie shufaa, mwaka ujao
ikibidi kuanzia sasa baada ya kuisoma makala hii, jenga tabia ya kusoma kazi za
wenzako, sisi hakika HATUANDIKI UPUMBAVU. Usituonee wivu kwamba ukituungisha
kitabu kimoja tutatoka kimaisha, vipi usiponunua na ukashuhudia tumetoka! Si
utatamani ufe kwa wivu. Tuungeni mkono jamani, ili kuandika kwetu tusiwe kama
tunapiga kwenzi kinyago tunaumiza vidole vyetu,
Huenda
umemsikia LAZARO SAMWELI wa chuo kikuu SAUT MWANZA anatangaza kitabu chake
kiitwacho NGUZO
TATU ZA MAISHA, Ivi wewe unadhani huyu jamaa atakuwa ameandika
UPUMMBAVU? Unazifahamu wewe hizo nguzo tatu za maisha? Huzijui ndio maana kila
siku unalia maisha magumu, hela haipatikani, mara unamlaumu Magufuli. Si uache
dharau uagize kitabu hicho cha NGUZO TATU ZA MAISHA
kama nilivoagiza mimi! Alaaaa!
Halafu
na huyu rafiki yangu BULIBA MAGAMBO, wa chuo kikuu cha DAR ES SALAAM ameanza
kutangaza kitabu chake kiitwacho HITIMU NA “A”-ZIJUE MBINU ZA KUWA BORA NA WA KWANZA
DARASANI. Chaajabu wewe ni mwanafunzi na kila siku masomo
yanakukamata unatamani umalize tu kusoma au uache na pengine darasani ndo hivo tena hali yako
mbaya, halafu unavoona kitabu kimeandikwa “HITIMU NA “A”-ZIJUE MBINU ZA KUWA
BORA NA WA KWANZA DARASANI.” Unapuuzia unanunua kilichoandikwa CHEMISTRY BOOK FOUR, unaakili wewe? Si uchukue
kwanza kinachokuelekeza mbinu za kusoma! Hata ujaze vitabu mabegi yako yote
uliyonayo shuleni halafu hujui namna ya kuvisoma ni kazi bure, ndugu yangu.
Sidhani kama bado hujanielewa!
Ila
naongezea, ukome kutudharau sisi waandishi, maana sisi HATUANDIKI
UPUMBAVU. Tunakaa chini tunatulia tukuase kitu fulani, wewe unatudharau.
Ebo! Vitabu vyenyewe sh.ngapi hivi, buku jero inakuuma hadi unaacha kununu
unaona bora ununu Safari lager ulewe upepesuke ujishushie heshima, nunua kitabu
wewe acha viroba!
AHSANTENI
SANA WAPENDWA…….!
No comments:
Post a Comment